VIJANA MSIKUBALI KUKATISHWA TAMAA MPAKA MKATISHA TAMAA AKATE TAMAA-MNEC TAIFA, KASESELA


VIJANA MSIKUBALI KUKATISHWA TAMAA MPAKA MKATISHA TAMAA AKATE TAMAA-MNEC TAIFA, KASESELA


Kutokana na vijana kuwa nguvu kazi ya Taifa,wametakiwa kuwapima wagombea wao kwa uadilifu na uzalendo ili watende haki katika kuleta maendeleo.

Akizungumza na wananchi katika sherehe za miaka 48 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mafinga Mkoani Iringa, MNEC Taifa Richard Kasesela amewataka vijana kuwachagua viongozi waadilifu na wapenda maendeleo kwani kufanya hivyo kutawafanya wasijutie kuwachagua.

"vijana mnaowajibu wa kuwachagua viongozi wazuri na wenye sifa za kuwa viongozi ili walete maendeleo katika maeneo yenu". Amesisitiza

Post a Comment

Previous Post Next Post